Windows

Simba kuanza na Arusha Fc kombe la FA



Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba wataanzia nyumbani raundi ya tatu ya michuano ya kombe la FA (ASFC)

Katika droo iliyofanyika mapema leo, Simba imepangwa kucheza na Arusha Fc kutoka mkoani Arusha

Mchezo baina ya timu hizo utapigwa uwanja wa Uhuru

Kwa misimu miwili mfululizo Simba haikuvuka raundi ya tatu lakini msimu huu uongozi umeweka wazi mapema kuwa wamepania kutwaa taji hilo

Hivyo michuano hiyo itapewa kipaumbele kama ilivyo michezo ya ligi

Michezo ya raundi ya tatu itapigwa kati ya Disemba 20-28 2019



Kwa habari zaidi Download App ya SOKA KIGANJANI kutoka Play Store.

Post a Comment

0 Comments