

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania Bara 'Kilimanjaro Stars' leo kimeemdelea na mazoezi kwenye uwanja wa Taifa kujiandaa na michuano ya CECAFA Chalenji inayofanyika kuanzia mwishoni mwa wiki nchini Uganda
Wachezaji saba wa Simba walijumuishwa katika kikosi cha timu hiyo kinachonolewa na kocha Juma Mgunda akishirikiana na Selemani Matola
Wote tayari wameripoti kambini na kushiriki kikamilifu mazoezi ya timu hiyo
Mlinda lango Aishi Manula anaongoza orodha ya nyota hao. Wengine ni Gadiel Michael, Mohammed Hussein, Jonas Mkude, Mzamiru Yassin, Hassan Dilunga na Miraji Athumani
Kilimanjaro Stars inatarajiwa kuondoka nchini keshokutwa Alhamisi kuelekea Uganda
Watacheza mchezo wa kwanza dhidi ya ndugu zao Zanzibar Heroes Jumapili, Disemba 08
Kwa habari zaidi Download App ya soka kiganjani kutoka Play Store.



0 Comments