Windows

Kuelekea uzinduzi wa Bunju Complex



Viwanja vya klabu ya Simba vilivyoko Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es salaam vimekamilika ambapo uzinduzi unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii

Baada ya kazi kubwa ya kutandika kapeti katika kiwanja cha nyasi bandia kwa sasa mafundi wanaendelea na zoezi la usafi pamoja na kurekebisha maeneo ambayo hayako sawa

Aidha kazi hiyo inaenda sambamba na ujenzi wa uzio

Hakika ni jambo la kuvutia, Mwekezaji wa Simba Mohammed Dewji, Bodi ya Wakurugenzi na viongozi wanastahili pongezi nyingi kwa kufanikisha ndoto hii ya Wanamsimbazi kumiliki uwanja wao ingawa kwa sasa ni kwa ajili ya mazoezi tu

Lakini kukamilika kwa awamu ya kwanza kunatoa nafasi kwa kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa awamu ya pili ambao utahusisha uwekaji wa majukwaa na Hostel za wachezaji



Kwa habari zaidi Download App ya SOKA KIGANJANI  kutoka Play Store.

Post a Comment

0 Comments