Windows

SIMBA: MAMBO BADO MAGUMU KWETU, KAZI IPO



UONGOZI wa Simba umesema kuwa kwa sasa hesabu zao kubwa ni kupata matokeo kwenye mechi zao zote zilizobaki licha ya ushindani mkubwa wanaoupata kwa sasa kwenye ligi.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mratibu wa Simba, Abas Abdalah amesema kuwa kikosi kipo imara na wanapambana kupata matokeo.

"Kwa sasa tupo vizuri na tuna kazi ngumu ya kufanya kwenye ligi kutokana na malengo ambayo tumejiwekea, ligi ni ngumu hilo lipo wazi ila tunapambana katika michezo yetu iliyobaki.

"Hakuna mchezaji ambaye ni mgonjwa kwetu zaidi ya Shomari Kapombe ambaye naye ameanza mazoezi wengine wote wapo fiti kwa ajili ya kupambana," amesema.

Simba kesho inashuka uwanjani kumenyana na Mbeya City mchezo utakaochezwa uwanja wa Sokoine.

Post a Comment

0 Comments