Windows

WAZIRI MSTAAFU ATAJA SABABU ZA KUREJEA NDANI YA CCM



WAZIRI Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Lowassa ambaye anapenda michezo ila ni msiri kuzungumzia timu anayoshabikia bongo, jana Ijumaa alitangaza kurejea ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) akitokea Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Lowassa ambaye alijiengua CCM mwaka 2015 baada ya jina lake kukatwa kwenye mchakato wa kuwania nafasi ya urais, alijiunga na CHADEMA mwaka huo na alipata nafasi ya kugombea nafasi ya urais kupitia chama hicho, alishindwa na mpinzani wake John Pombe Magufuli kutoka CCM.

Baada ya kurejea CCM, Lowassa amepokelewa na Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam.

Baada ya kupokelewa kwake jana Lowassa alisema kwa kifunpi sababua ya kurehea ndani ya CCM kwamba "Narejea nyumbani, nimerejea nyumbani, haitoshi CCM oyee," alisema Lowassa.

Post a Comment

0 Comments