

Wakati Wanamsimbazi wakisubiri taarifa rasmi ya viongozi wao kuhusu kocha mpya, kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Zambia Sven Van Der Broeck anatajwa kuwa yuko nchini akihusishwa na nafasi hiyo
Kocha huyo kijana inaelezwa kuwa huenda ndiye atakayetangazwa kuwa mkufunzi wa Simba
Van Der Broeck raia wa Ubelgiji hana jina kubwa sana lakini ni kocha anayeonekana kuyakimbilia mafanikio kwa kasi kubwa
Kwani katika umri mdogo (miaka 40) tayari amepata nafasi ya kuaminiwa kupewa majukumu ya kufundisha timu za Taifa
Simba jana ilimtangaza Selemani Matola kuwa kocha msaidizi huku kukiwa na taarifa kuwa kocha mkuu huenda akatangazwa leo
Je ni Van Der Broeck au Chambeshi? tusubiri..
Kwa habari zaidi Download App ya Mwana Msimbazi kutoka Play Store



0 Comments