Windows

Simba kuendelea na mazoezi Jumanne



Pamoja na mkanganyiko wa ratiba, kikosi cha Simba kinatarajiwa kuendelea na mazoezi kesho Jumanne baada ya mapumziko ya siku mbili

Mabingwa hao wa Tanzania Bara hawaonekani kuwa na mchezo hadi January 04 2020 watakapo-wakabili watani zao Yanga katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa

Baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Ruvu Shooting juzi, wachezaji walipewa mapumziko hayo

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema benchi la ufundi litaandaa program maalum ya mazoezi wakati wote ambao ligi itakuwa imesimama kupisha michuano ya CECAFA Chalenji inayoanza Disemba 07 nchini Uganda

Ligi hiyo inaendelea kwa mechi tatu kpigwa katika viwanja mbalimbali;

Post a Comment

0 Comments