

DR Congo ya Mwinyi Zahera ilishinda mabao 4-0 kwenye mchezo huo na kufuzu jambo ambalo liliibua mijadala mingi.
Habari zilimhusisha Katumbi na kipa wa Zimbabwe kwamba amempa mshiko ili alegeze jambo ambalo amelikana na tayari amepeleka utetezi wake Caf.
Kupitia ujumbe wake kwenye Twitter yake, Katumbi amesisitiza madai hayo ni ya hovyo na kwamba hata siku mechi hiyo inachezwa hakuwepo Misri alisharudi zake Congo.
Kiongozi huyo mwenye heshima kwenye soka la Afrika amesisitiza kwamba hawezi kuhusika kwenye mambo ya hovyo kama hayo ya kupanga matokeo. Huku uchunguzi ukiendelea, DR Congo itacheza na Madagascar leo Jumapili kwenye mechi ya 16 Bora




0 Comments