

Uongozi wa Azam Fc umetangaza kuachana na nyota wake nane baada ya kuwa wamemaliza mikataba
Miongoni mwa wachezaji hao waliopewa mkono wa kwaheri ni pamoja na mshambuliaji Obrey Chirwa ambaye wameshindwa kufikia nae makubaliano upande wa mshahara
Winga wa zamani wa Simba Ramadhani Singano 'Messi' nae ameachwa
Wengine waliotemwa ni Joseph Kimwaga, Hassan Mwasapili, Enock Atta Agey, Twafazwa Kutinyu (amejiunga Horoya AC), Steven Kingu na Danny Lyanga



0 Comments