Windows

Simba yapania kumalizana na Kahata mapema


Ishu ya usajili wa kiungo wa Gor Mahia Francis Kahata sio tetesi tena kwani kiungo huyo anatarajiwa kuwasili nchini wakati wowote kusaini mkataba wa kuitumikia Simba, imefahamika

Taarifa za uhakika ni kwamba tayari kiungo huyo anayemaliza mkataba kuitumikia Gor Mahia ameshatumiwa tiketi ya Ndege ili aje kumalizana na mabingwa hao wa Tanzania Bara

Simba inataka kumsajili Kahata kabla hajaingia timu ya Taifa ya Kenya ambayo itasafiri nchini Ufaransa kwenda kuweka kambi kujiandaa na fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika nchini Misri mwezi ujao

Mmoja wa viongozi waandamizi wa Simba amethibitisha Kahata kutumiwa tiketi ya Ndege akitarajiwa kuwasili nchini kabla ya Jumamosi

Jana Mtendaji wa Simba Crescentius Magori alisema wanafahamu Kahata anamaliza mkataba Gor Mahia na ameshaaaga timu hiyo kuwa hataongeza mkatabacut

Hata hivyo Magori hakuweza wazi kama Simba tayari imeanza mchakato wa kumsajili

Usajili wa Kahata unatajwa kuja kuimarisha zaidi safu ya kiungo katika ushambuliaji

Kwa sasa Simba inawategemea Clatous Chama, Haruna Niyonzima na Hassani Dilunga

Post a Comment

0 Comments