![](https://4.bp.blogspot.com/-oWBF5rnYXzE/W7uedCj85EI/AAAAAAAAJdY/0jTfLk_9khU5DTaZ6o-KfH_A3hrpI_ZJQCLcBGAs/s320/aaaaaaaaaa.jpg)
![](https://1.bp.blogspot.com/-5UdUkBxLqPE/W7ujeNJL4XI/AAAAAAAAJds/dBugYDvLQq0WptS1YBXQGjJB_vJFBWL7wCLcBGAs/s320/yyyyyyyyyyyy.jpg)
![](https://www.mwanaspoti.co.tz/image/view/-/5119770/highRes/2346607/-/maxw/600/-/rc69tsz/-/NGOMA+PIC.jpg)
“Sina maana kwamba hakuna wachezaji wazuri katika klabu hizo, ila hawatamani kucheza Azam kwani haina mashabiki wengi na tayari wamelewa sifa wanafurahia mashabiki wanavyowapa kipaumbele zaidi na kusahau kuwa, kuna maisha mengine nje ya ushabiki.
“Kwa sasa huwezi ukamtoa mtu kama Ibrahim Ajibu aje Azam inayotegemea soka la uwanjani na sio mashabiki, ndio maana nasema hakuna anayeweza kuja kucheza huku kama hujitambui.” alisema Ngoma aliyefunga mabao 37 katika Ligi Kuu kwa misimu minne kuanzia mwaka 2015. Ngoma alisema amecheza Yanga na sasa yupo Azam na ameona tofauti kubwa baina ya klabu hizo, ila anafurahia kipaji chake kinachomfanya ajiachie kwa raha akifurahia maisha ya soka bila kujali kama kuna mashabiki wanamfuatilia au la.
![](https://4.bp.blogspot.com/-oWBF5rnYXzE/W7uedCj85EI/AAAAAAAAJdY/0jTfLk_9khU5DTaZ6o-KfH_A3hrpI_ZJQCLcBGAs/s320/aaaaaaaaaa.jpg)
![](https://1.bp.blogspot.com/-5UdUkBxLqPE/W7ujeNJL4XI/AAAAAAAAJds/dBugYDvLQq0WptS1YBXQGjJB_vJFBWL7wCLcBGAs/s320/yyyyyyyyyyyy.jpg)
![](https://1.bp.blogspot.com/-5UdUkBxLqPE/W7ujeNJL4XI/AAAAAAAAJds/dBugYDvLQq0WptS1YBXQGjJB_vJFBWL7wCLcBGAs/s320/yyyyyyyyyyyy.jpg)
0 Comments