![](https://4.bp.blogspot.com/-oWBF5rnYXzE/W7uedCj85EI/AAAAAAAAJdY/0jTfLk_9khU5DTaZ6o-KfH_A3hrpI_ZJQCLcBGAs/s320/aaaaaaaaaa.jpg)
![](https://1.bp.blogspot.com/-5UdUkBxLqPE/W7ujeNJL4XI/AAAAAAAAJds/dBugYDvLQq0WptS1YBXQGjJB_vJFBWL7wCLcBGAs/s320/yyyyyyyyyyyy.jpg)
UONGOZI wa Simba umemkingia kifua nahodha wa timu hiyo John Bocco kwa kushindwa kutumia nafasi za wazi ambazo anazipata akiwa kwenye mechi za ushindani.
Bocco hivi karibuni katika mchezo wa Ligi Kuu Bara alikosa kutumia vema nafasi tatu alipokuwa na mlinda mlango wa Mwadui FC, pia katika mchezo wa kimataifa dhidi ya Al Ahly uliochezwa Uwanja wa Taifa Bocco alikosa nafasi mbili za wazi kupachika mabao.
Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema ni watu wachache wanaoelewa kitu anachofanya Bocco akiwa Uwanjani na kumlaumu anapokosa magoli.
"Wakati mwingine tunapomlaumu kwa kukosa magoli tuangalie shughuli yake kwa mabeki wa timu pinzani, ni mwadamu pekee ambaye amefunga zaidi ya goli mia katika ligi anastahili heshima.
"Amehusika katika kumtengenezea bao Kagere (Meddie) pia bao lake la penalti pale kitwe (Nkana) lilitupa nguvu ya kufuzu makundi, nahodha wangu bora wadhibitishie namna ulivyo, najua utafanya hivi karibuni," amesema Manara.
![](https://4.bp.blogspot.com/-oWBF5rnYXzE/W7uedCj85EI/AAAAAAAAJdY/0jTfLk_9khU5DTaZ6o-KfH_A3hrpI_ZJQCLcBGAs/s320/aaaaaaaaaa.jpg)
![](https://1.bp.blogspot.com/-5UdUkBxLqPE/W7ujeNJL4XI/AAAAAAAAJds/dBugYDvLQq0WptS1YBXQGjJB_vJFBWL7wCLcBGAs/s320/yyyyyyyyyyyy.jpg)
![](https://1.bp.blogspot.com/-5UdUkBxLqPE/W7ujeNJL4XI/AAAAAAAAJds/dBugYDvLQq0WptS1YBXQGjJB_vJFBWL7wCLcBGAs/s320/yyyyyyyyyyyy.jpg)
0 Comments