Windows

Kocha Mpya Simba kuzungumza na Wanahabari Ijumaa




Kocha Mkuu wa Simba Sven Vanderbroeck atazungumza na Wanahabari siku ya Ijumaa Disemba 13 kuweka hadharani mipango yake

Simba imemtambulisha Vanderbroeck leo na atashirikiana na kocha msaidizi Selemani Matola

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amesema Simba imempa majukumu kocha huyo kwa kuwa malengo yake yanafanana na ya timu

"Huyu ni Kocha kijana mwenye malengo yanayofanana na malengo ya klabu yetu," amesema Manara

"Huyu ameshashinda Ubingwa wa Afcon akiwa kocha msaidizi wa Cameroon na ameshafundisha wachezaji Wakubwa"

"Pia keshakuwa kocha mkuu wa Zambia na alikuwepo kitwe mwaka jana tulipocheza na Nkana, anayajua malengo yetu na nini tunakitaka"

"Ijumaa ataongea na Wanahabari kuelezea mipango na matarajio yake kwa Machampioni wa taifa hili"

Post a Comment

0 Comments