Windows

Simba yajifua bila Aussems



Baada ya mapumziko ya siku mbili, kikosi cha Simba leo kimerejea mazoezini kuendelea na maandalizi ya michezo ya ligi inayofuata

Simba imejifua bila ya kocha wake Mkuu Patrick Aussems ambaye amesimamishwa akisubiri maamuzi ya kikao cha Kamati ya Nidhamu na Maadili ambacho kitakaa keshokutwa Alhamisi

Kocha Msaidizi Denis Kitambi pamoja na maafisa wengine wa benchi la ufundi walisimamia mazoezi hayo yaliyofanyika uwanja wa Gymkhana jijini Dar es salaam

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mazoezi hayo, Kitambi amesema wamefanya mazoezi ya kawaida kuweka miili sawa

Amesema bado hawajaandaa program ambayo wataitumia kipindi hiki ambacho ligi itasimama kwa mwezi mzima kupisha michuano ya CECAFA Chalenji

KUPATA HABARI MPYA KILA WAKATI PAKUA APP YA  ......SOKA KIGANJANI

Post a Comment

0 Comments