Windows

Molinga, Balinya wapewa kazi maalum Yanga




Mabadiliko yameanza kuonekana kwenye kikosi cha Yanga tangu kocha Charles Mkwasa alipokabidhiwa majukumu baada ya uongozi wa timu hiyo kulivunja benchi lote la ufundi

Mkwasa alitangazwa kuwa kocha wa muda kuanzia Novemba 05 mwaka huu baada ya Zahera pamoja na benchi lake lote la ufundi kuondolewa

Kocha huyo wa zamani wa timu ya Taifa, aliipokea Yanga ikiwa na changamoto nyingi, alilazimika kubadilisha mambo kadhaa ambayo yanaonekana kuisaidia timu hiyo

Mabadiliko hasa ya mfumo wa uchezaji yameifanya Yanga ifunguke zaidi na kutengeneza nafasi nyingi

Timu sasa haitegemei sana kufunga mabao yake kupitia mipira iliyokufa au kona

Katika michezo miwili iliyopita, Yanga imefunga mabao manne kawaida na mabao mawili kupitia mipira ya adhabu

Mkwasa anaonekana kujenga 'combination' mpya ya washambuliaji akitumia pacha ya Juma Balinya na David Molinga

Katika mchezo dhidi ya JKT Tanzania, Balinya na Molinga walianza pamoja ambapo wote walifanikiwa kufunga mabao kabla ya Molinga kutolewa kipindi cha pili

Wawili hao wamekuwa wakicheza pamoja hata mazoezini ikiwa ni ishara kuwa Mkwasa amewaamini na kuwapa jukumu la kuifungia timu hiyo mabao

Mshambuliaji Sadney Urikhob raia wa Namibia yeye hakujumishwa kabisa kwenye kikosi kilichoikabili JKT Tanzania

Huenda akabadilishiwa majukumu na kuanza kutumika akitokea pembeni badala ya mshambuliaji wa kati kama ilivyokuwa wakati wa Zahera

Post a Comment

0 Comments