


Ngorongoro Heroes leo Oktoba 10, 2019 imetwaa taji la CECAFA chini ya miaka 20 kwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kenya.
Bao hilo pekee limepatikana mnamo dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza kwa Otieno Onyango kujifunga.
Ushindi huo unaipa rasmi Tanzania kikombe hicho ambacho mashindano yake yalikuwa yanafanyika nchini Uganda.
Baada ya ushindi huo, Ngorongoro watarajia kurejea nchini kuanzia kesho.

The post Tanzania Yaitandika Kenya 1-0 Cecafa U20, Yatwaa Kombe appeared first on Global Publishers.



0 Comments