Windows

Bui amefuta machungu ya Zambia




Septemba 28 ilikuwa siku mbaya sana kwa kiungo Abdulaziz Makame 'Bui' ambaye goli alilojifunga nchini Zambia lilipelekea Yanga kuchapwa mabao 2-1 na Zesco na kupelekea kuondoshwa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Katika michezo miwili aliyocheza kwenye ligi, Bui amekuwa mchezaji anayejituma zaidi kwenye kikosi cha Yanga

Timu inaposhambulia anaongeza nguvu na timu inaposhambuliwa yuko katika ulinzi

Leo juhudi zake zimezaa natunda kwani amemaliza machungu ya nchini Zambia baada ya kuifungia Yanga bao muhimu lililowahakikishia mabingwa hao wa kihistoria ushindi wao wa kwanza msimu huu

Bui ametoa zawadi bao hilo kwa mashabiki wote ambao wameendelea kumuunga mkono na kusahau tukio la Zambia

Post a Comment

0 Comments