Windows

Kahata, Kanda kukabidhiwa jukumu la Okwi



Msimu uliopita safu ya ushambuliaji ya Simba iliyokuwa ikiundwa na Meddie Kagere, John Bocco na Emmanuel Okwi ilikuwa moto wa kuotea mbali

Washambuliaji hao walifunga mabao 53 kwenye ligi

Hata hivyo Simba imeanza kampeni msimu huu ikiwa na washambuliaji wawili Meddie Kagere na John Bocco baada ya Okwi kutimkia Misri



Katika mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa dhidi ya UD Songo, Bocco na Kagere walianza pamoja huku Francis Kahata na Clatous wakiungana nao wakitokea pembeni

Hata hivyo kocha Mkuu wa mabingwa hao wa nchi Patrick Aussems amekiri bado hajapata mtu sahihi wa kuziba nafasi ya Okwi

Akizungumza jana kwenye mazoezi ya Simba yaliyofanyika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es salaam, Aussems alisema anawaangalia Deo Kanda na Francis Kahata ili kutengeneza muunganiko na Bocco na Kagere

Amesema kwa uwezo unaoonyesha na wachezaji hao, anaamini baada ya muda safu ya ushambuliaji ya Simba itarejesha makali yake ya msimu uliopita

Post a Comment

0 Comments