


WINGA wa timu ya African Lyon iliyoshuka daraja kutoka Ligi Kuu Tanzania Bara hadi Daraja la kwanza, Hood Mayanja, yupo mbioni kutua Namungo FC.
Mchezaji huyo ambaye ni raia wa Uganda, huenda msimu ujao akakipiga kwa vijana hao kutoka Ruangwa ambao wamepanda Ligi Kuu Bara msimu iliomalizika hivi karibuni.
Habari kutoka Namungo FC, zinadai katika kuhakikisha kikosi kinaingia ligi kuu kikiwa imara, wameona ni vizuri kumsajili mchezaji huyo ambaye kwa sasa yupo huru.



0 Comments