Windows

Simba wanapewa ubingwa wao Morogoro leo


Shamrashamra za ubingwa wa ligi kuu zitakuwa mkoani Morogoro ambapo mabingwa wa msimu wa pili mfululizo, Simba watakabidhiwa kombe baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar

Mgeni rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri, ni Mh Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani

Mashabiki wa Simba mkoani Morogoro wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi katika hafla hiyo itakayofanyika saa 11 jioni baada ya kumalizika mchezo unaotarajiwa kuanza saa tisa Alasiri

Uwanja wa Jamhuri leo utapendeza kwa rangi nyekundu na nyeupe kwani ukiacha mashabiki wa Simba wa mkoani Morogoro, wapo mashabiki kutoka mikoa ya Dodoma, Singida na kutoka jijini Dar es salaam ambao tayari wako Morogoro

Huo ni ubingwa wa 20 kwa Simba

Aidha timu zote 20 zinatarajiwa kushuka dimbani leo kukamilisha msimu

Mechi zote zitapigwa muda mmoja (saa kumi) isipokuwa mchezo kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Simba ambao utaanza saa tisa Alasiri

Post a Comment

0 Comments