

Kiungo wa Yanga Thabani Kamusoko ni miongoni mwa wachezaji 34 walioitwa kuunda kikosi cha awali cha timu ya Taifa ya Zimbabwe kitakachoshiriki fainali za AFCN 2019 zitakazofanyika nchini Misri kuanzia Juni 21 2019
Kamusoko tayari amejiunga na timu hiyo itakayoshiriki michuano ya COSAFA kabla ya baadhi ya wachezaji kuchujwa kwa ajili ya michuano ya AFCON
Kiungo wa Azam Fc Tafadzwa Kutinyu nae ameitwa kwenye kikosi cha timu hiyo, huku Donald Ngoma mshambuliaji wa Azam akishindwa kupata nafasi
Kamusoko amesema michuano hiyo ni fursa kwake, itamuimarisha zaidi na kumfanya arejee akiwa imara msimu ujao
Hatma ya kiungo huyo kuendelea kubaki Yanga itafahamika wiki ijayo



0 Comments