Windows

ZAHERA ASEMA YANGA HAITEGEMEI TAJIRI MMOJA, KAULI ZAKE NNE NZITO HIZI HAPA


Kauli nne nzito alizozingumza Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera kuhusiana na klabu.

"Katika muda niliofanya kazi hapa, nimesoma na kujifunza vitu vingi sana hata kwa hiki nnachoshuhudia leo hakika kimenipa hamasa sana! msimu ujao hatutoumia.

Nimetembea karibu nchi zote za Afrika nikiwa na timu ya Taifa, nawahakikishieni hakuna hata nchi moja yenye mashabiki kama hawa wa Yanga, hata TP Mazembe haina fanbase kubwa kama Yanga. .

Najiuliza kuna ulazima gani timu kama hii eti kungoja tajiri mmoja aje awekeze pesa zake wakati wenyewe mnasema hii ni timu ya wananchi?

"Kwanini wananchi tusiibebe timu yetu wenyewe? Sasa tunapaswa kuibeba wenyewe, timu kama Yanga SC inapaswa kushindania makombe makubwa Afrika. Naomba tuichangie Yanga"

Post a Comment

0 Comments