Windows

BAADA YA KUWA KIMYA TANGU ATUE NCHINI, ZANA ATOA TAMKO LAKE RASMI SIMBA


Beki Zana Coulibally amewashukuru mashabiki wa Simba ambao walionyesha kumuunga mkono wakati akiendelea kurejea katika kiwango chake.

Zana amefanya hivyo mara tu baada ya mechi dhidi ya Yanga na Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Meddy Kagere.

Mara tu baada ya mechi, Zana aliwafuata mashabiki wa Simba na kuwaonyesha ishara ya shukurani na baadaye kusema, walimvumilia na sasa ameanza kupata kiwango chake.

Baada ya kutua nchini, Zana alikuwa gumzo akionekana hana kiwango kizuri kama ambavyo wengi walitarajia.

Hata hivyo ilielezwa hakuwa katika kiwango kizuri kwa kuwa hakuwa amecheza kwa muda mrefu

Post a Comment

0 Comments